Monday, January 30, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 30

SIKU YA 30 - 30/01/2017

NINAMSHUKURU BWANA, NAMPA DHABIHU ZA KUSHUKURU

Zaburi 50:14 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru; Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.
Zaburi 50:23 Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonyesha wokovu wa Mungu.

Zaburi 54:6 Kwa ukunjufu wa moyo nitakutolea dhabihu; Ee Bwana, nitalishukuru jina lako, maana ni jema.

Zaburi 56:12 Ee Mungu, nadhiri zako zi juu yangu; Nitakutolea dhabihu za kushukuru.

Zaburi 107:22 Na wamtolee dhabihu za kushukuru, Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba.

Zaburi 116:17 Nitakutolea dhabihu ya kushukuru; Na kulitangaza jina la Bwana;

Yona 2:9 Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani; Nitaziondoa nadhiri zangu. Wokovu hutoka kwa Bwana.

Amosi 4:5 mkachome sadaka ya shukrani, ya kitu kilichotiwa chachu; mkatangaze sadaka mtoazo kwa hiari na kuzihubiri habari zake; kwa maana ndivyo viwapendezavyo ninyi, enyi wana wa Israeli, asema Bwana MUNGU.

KAMA UMEPITIA MISTARI HIYO, KUNA MAMBO KADHAA YANAAMBATANA NA KUSHUKURU

1… KUONDOA NADHIRI ZAKO KWA BWANA….

2… KUTENGENEZA MIENENDO YAKO….

3… KUYASIMULIA MATENDO YAKE…

4… KULITANGAZA JINA LAKE…

5… KUIMBA…

6… KUTOA SADAKA ZA HIARI…

KWA UFUPI NI TENGENEZA MAMBO YAKO YA NDANI- NYUMA YA PAZIA (Kama una njia ambazo unajua hazimpendezi BWANA, NA KUSHUHUDIA WENGINE MATENDO MAKUU YA MUNGU, WOKOVU WAKE N.K.)
2 Mambo ya Nyakati 33:16 Akaijenga madhabahu ya Bwana, akatoa juu yake dhabihu za sadaka za amani, na za shukrani, akawaamuru Yuda wamtumikie Bwana, Mungu wa Israeli.

SADAKA YA SHUKRANI INAWEZA KUWA YA MANENO/WIMBO (Nehemia 12:46, Yona 2:9, Yeremia 30:19) AU MALI (2 Nyakati 33:16) AU VYOTE (2 Wakorintho 9:11) inategemea msisitizo wa Roho Mtakatifu ndani yako…

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

No comments:

Post a Comment