Monday, January 30, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 28

SIKU YA 28 - 28/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

EE BWANA NIKO TAYARI KUONGOZWA NA WEWE = MPANGO WAKO UWE WANGU
Mara nyingi tunakuwa na mipango yetu mizuri sana (ni muhimu sana kupanga na kuwa na malengo) LAKINI Mungu ndiye anayejua kiasi gani mipango yetu imenyooka au kupinda, yanapoteza au tumepatia… Hivi karibuni nimegundua kwamba kila nilipoomba maelekezo kwa njia ya maombi kuna mambo mengi Mungu ameyabatilisha tofauti na nilivyopanga.. LAKINI mabadiliko hayo yamenipa matokeo ambayo sikuyapata kwa KUHENYA/ NO STRESS

Unajua huwa hatuombi ili tumfanye Mungu abadili mawazo yake na kufuata ya kwetu? Tunaomba ili tuweze kujua na kufuata mpango thabiti aliyoweka kwa ajili yetu…

Isaya 55:8 Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.

NI SAWA KABISA, LAKINI NAPENDA MAWAZO (PLANS) YA MUNGU KWANI YAKO JUU SANA..

Isaya 55:9 Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.


UHONDO NI PALE TUNAPOPANGA MAWAZO YA KUTUFANIKISHA KUMBE MUNGU NAYE ANA MPANGO HUO HUO…

Kama LENGO ni KUFANIKIWA Mungu naye hayuko mbali na MPANGO wa kutimiza hilo lengo..

Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo [PLANS] ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani [PROSPERITY] wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho. [FUTURE]

Pale neno MAWAZO limetumika kama PLANS = MIPANGO…

Haya MAWAZO/MIPANGO Bwana anaweza kutufundisha kabisa

Zaburi 32:8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.

NA LENGO LAKE LA KUTUFUNDISHA NI KUTUFAIDISHA………… HALELUYAH……

Isaya 48:17 Bwana, mkombozi wako, mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata.

MUNGU HATAKI TUPITE NJIA AMBAZO HATUPASWI KUPITA KABISA… SIYO KILA MPANGO NI WA KUFUATA HATA KAMA WAONEKANA MZURI KWA MACHO NA AKILI nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata
EE BWANA, NINAOMBA UNIFUNDISHE MIPANGO YAKO YENYE FAIDA, NIONYESHE MKAKATI ULIONAO JUU YA MAISHA YANGU, MAWAZO/MIPANGO YAKO IWE MPANGO YANGU, NAREJESHA MIPANGO YANGU YA 2017 CHINI MAPITIO YAKO, UYACHUNGUZE NA KUONDOA LOLOTE LENYE KULETA HASARA/KUANGAMIZA, NITAPITA TU NINAPOPASWA, EE BWANA NISAIDI KWANI Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti [Mithali 14:12, Mithali 16:25] NAMI SITAKI KUPITA HUKO, KATIKA JINA LA YESU

UNAWEZA KUOMBA MAOMBI HAYA JUU YA MKE/MUME WAKO, RAFIKI, NDUGU, AU MTU YEYOTE AMBAYE KILA AKIPANGA MAMBO YANAMWENDEA KOMBO KATIKA JINA LA YESU ATAPATA MPENYO KATIKA MAISHA YAKE…

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

No comments:

Post a Comment