Friday, January 27, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 27

SIKU YA 27 - 27/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA


EE BWANA, NISAIDIE KUTOKUAMINI KWANGU

Umewahi kumwamini Mungu kukufanyia jambo Fulani, mwanzoni halafu baadaye unaona huwezi tena kushikilia Imani yako?

Umewahi kuamini Mungu kufanyia jambo kubwa lakini baadaye hali inakuwa tofauti na kuamini hata KUTAKA au kuamua kubadili ukiri wa Imani yako?

Umewahi kuamini jambo kubwa lakini siku zinavyozidi kwenda mbele, umeanza kushusha kiwango ulichokuwa unataka? Au hata kuomba.. Aaah! Vyovyote itakavyotokea I don’t care?

WAKATI MWINGINE IMANI YAKO INATIKISWA KWELI KWELI MPAKA UNAHISI INANG’OKA KABISA…

Maandiko yanasema Waebrania 11:13 Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, na kukiri kwamba walikuwa wageni, na wasafiri juu ya nchi.

Badala ya kukata tamaa…. AMINI HADI KUFA WALA USIBADILI UKIRI WAKO… Imani haiko juu ya kile unachokiona bali kwa Mungu na Mungu aweza kufanya lolote kwa wakati wowote… kujidhihirisha kwamba yeye ni Mungu… 

Baba yake kijana aliyekuwa anateswa na mapepo alimwambia Yesu Marko 9:24 …. Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.

CHA AJABU YESU ALIMSAIDIA…. …… akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena.
HATA PETRO ALIPOANZA KUTEMBEA JUU YA MAJI… Akaona mazingira yakamtia hofu na akaanza kupoteza Mathayo 14:29-31 Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe. Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?

WAKATI WOWOTE KWENYE MAISHA UNAPOINGIA KATIKA MASHAKA NA IMANI YAKO HAIWEZI KUSHIKA NETWORK VIZURI…. Mwambie Yesu… niokoe, ninazama nikijiona…
Sijawahi kuona rafiki kama Yesu HATA IMANI ZETU ZINAPOTINDIKIWA HAJAWAHI KUSHINDWA KUTUSAIDIA…

ANGALIA MADHARA YA KUTOKUAMINI……… Mathayo 13:58 Wala hakufanya miujiza mingi huko, kwa sababu ya kutokuamini kwao.

TENA ANASTAAJABU TUSIPOAMINI Marko 6:6 Akastaajabu kwa sababu ya kutokuamini kwao.

TAARIFA SAHIHI NI MUNGU ANAPENDA SANA KUTUSAIDIA KATIKA HALI ZETU IJAPOKUWA ATAKEMEA UPUNGUFU WA IMANI ZETU…

EE BWANA YESU…NISAIDIE KUTOKUAMINI KWANGU KATIKA (……………..Taja hayo mambo)….

IMANI YA YESU IWE IMANI YANGU….. KUMBUKA HATUAMINI KWENYE MATOKEO.. TUNAAMINI KWA MLETA MATOKEO…. MUNGU… NA YEYE ANADUMU WA KUAMINIWA…
NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu
Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

No comments:

Post a Comment