Friday, January 27, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 26

SIKU YA 26 - 26/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

NAKATAA KUISHI KAMA WA ULIMWENGU HUU, MIMI NI RAIA WA MBINGUNI

Kuna changamoto kubwa sana mtoto wa ufalme wa Mungu anavyoishi na kuamua kuishi mfumo wa maisha yanayofanana na mtoto wa ulimwengu… MATATIZO YAO YANAFANANA, MIFUMO YA MAISHA, AINA YA MALALAMIKO, AINA ZA MAJANGA, N.K… 

TAARIFA: WEWE SI WA ULIMWENGU HUU

Angalia Yesu anachosema kwenye maombi yake akituombea. Yohana 17:9 Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako

UKIMPOKEA YESU… UMEKABIDHIWA KWA YESU… NA ULIMWENGU HAUKUTAMBUA HATA KAMA UNAISHI HUMO.. Akanongeza kusema… wao wanatakiwa kuongozwa na NENO la Kristo na siyo wa ulimwengu… 

Yohana 17:14 Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama mimi nisivyo wa ulimwengu.

Sasa kama sisi siyo wa huku, Kwa nini tusiende kwetu..? YESU ALIJIBU HILO… Yohana 17:18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo naliwatuma hao ulimwenguni. WE ARE HERE FOR A MISSION.. SISI NI MABALOZI WA UFALME WA MUNGU (NYUMBANI KWETU)

TENA YOHANA AKAONGEZA KWENYE BARUA YAKE… 1 Yohana 4:4 Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia. NDIYO MAANA PAULO AKASEMA Warumi 12:2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamili KUGEUZWA UPYA NIA KWENYE KUFUATA NAMNA (PATTERNS) ZA DUNIA HII BALI NENO LA MUNGU LIWE ….. taa ya miguu ZETU, Na mwanga wa njia ZETU. Zaburi 119:105

ANGALIA JINSI WANA ISRAELI WALIVYOTOFAUTISHWA….NA ULIMWENGU MWINGINE… HII NI PICHA HALISI YA MAISHA YETU…

Mwanzo 47:27 Israeli akakaa katika nchi ya Misri, katika nchi ya Gosheni. Wakapata mali humo, wakaongezeka na kuzidi sana

Walipokaa Gosheni waliongezeka na kuzidi sana JUST IMAGINE

NA PINDI MAJANGA YALIPOACHILIWA KATIKA NCHI… WALITOFAUTISHWA… Kutoka 8:22 Nami siku hiyo nitatenga nchi ya Gosheni, watu wangu wanayokaa, ili hao mainzi wasiwe huko; ili kwamba upate kujua wewe ya kuwa mimi ndimi Bwana kati ya dunia KWA HIYO MUNGU ANAJIONYESHA KUWA NI MUNGU KWA KUWATENGA NA MAJANGA YA MISRI…

HATA MVUA YA MAWE ILIVYOPIGA PIA…IMEANDIKWA… Kutoka 9:26 Katika nchi ya Gosheni peke yake, walikokaa wana wa Israeli, haikuwako mvua ya mawe

JE, WAJUA Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Mathayo 5:14 NA NDIYO MAANA ULIMWENGU UNAWEZA KUWACHUKIA KAMA WAMISRI WALIVYOFANYA KWA WAISRAELI Yohana 15:18 Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.

NDIYO MAANA KUNA MAJIPU YA MISRI ILA HAKUNA MAJIPU YA ISRAEL Kumbukumbu la Torati 28:27 

WAKATI FULANI TUNAJISAHAU AU HATUKUJUA YA KUWA TUNAWEZA KUJITENGA NA MAJANGA YANAYOIKUMBA DUNIA KWA KUAMUA KUFUATA MFUMO WA NENO LA MUNGU KWA UONGOZI WA ROHO MTAKATIFU….

EE BWANA KWA ROHO WAKO MTAKATIFU, NISAIDIE KUISHI KAMA mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, ILI kuzitangaza fadhili zako wewe uliyeniita nitoke gizani nikaingia katika nuru yako ya ajabu, nisiishi kwa kufuatisha namna ya dunia, malalamiko yao, shida zao, changamoto zao. Bali niwe chachu ya kuwasaidia, kuwapa mwanga, niwe jibu la matatizo yao, magonjwa yao, tabu zao, n.k.. niishi kifalme (wa mbinguni) nikitangaza HAKI YAKE, AMANI YAKE, NA FURAHA KATIKA ROHO MTAKATIFU

WE ARE NOT AFFECTED, WE AFFECT. WE ARE AMBASSADORS OF HEAVEN ON EARTH

NB: KAMA HUJAOKOKA MALIZANA NA HIYO BIASHARA.. *MPE YESU MAISHA YAKO KWANZA

NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU 

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu
Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

No comments:

Post a Comment