Tuesday, January 24, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 24

SIKU YA 24 - 24/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

BWANA, NISAIDIE KUONA NA KUTUMIA NILIVYONAVYO

Changamoto na malalamiko ya watu wengi leo ni kudharau vitu walivyonavyo tayari. Watu wengi wanahisi wanakwama kwa sababu hawana baadhi ya vitu.. utasikia mtu akisema sina elimu ya kutosha, sina mtu wa kuniunganishia dili, sina rangi nzuri, sina alama za kuniwezesha, sina mama wa kunishauri, sina mtaji wa kuanza nayo…. NA MUNGU ANAWATAZAMA KWA MSHANGAO AKISEMA NANI ALIYEMWABIA HUYU KAMA VILIVYOKO NJE NDIYO VINAMKWAMISHA?

SINA MKATE, ILA KONZI YA UNGA KATIKA PIPA, NA MAFUTA KIDOGO KATIKA CHUPA

1 Wafalme 17:12 Naye akasema, Kama Bwana, Mungu wako, aishivyo, sina mkate, ila konzi ya unga katika pipa, na mafuta kidogo katika chupa; nami ninaokota kuni mbili ili niingie nijipikie nafsi yangu na mwanangu, tuule tukafe.

HUYU MJANE ALIONA HAPA ALICHONACHO HAKIWEZI KUMSAIDIA NA MARA NYINGI HATUTEGEMEI KUZALISHA TULIVYONAVYO BALI KUZITUMIA NA KUFIA MBELE…

SINA KITU NYUMBANI, ILA CHUPA YA MAFUTA

2 Wafalme 4:2 Elisha akamwambia, Nikufanyie nini? Niambie; una kitu gani nyumbani? Akasema, Mimi mjakazi wako sina kitu nyumbani, ila chupa ya mafuta.

ALIDHARAU KWANZA CHUPA YA MAFUTA AMBAYO INGETUMIKA KULIPA MADENI YAKE… KUMBUKA HATA HAKUONA UMUHIMU WA WALE WATOTO WAKE… 2 Wafalme 4:1 ….. akasema, Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha Bwana; na aliyemwia amekuja ili ajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa. LAKINI HUYO ANAYEMDAI ALIONA FURSA YA KUWATUMIA HAO WATOTO WA MJANE….

ALIPOTUMIA USHAURI WA ELIYA 2 Wafalme 4:7 Ndipo akaja akamwambia yule mtu wa Mungu. Naye akasema, Enenda ukayauze mafuta haya, uilipe deni yako; nayo yaliyosalia uyatumie wewe na watoto wako.

ALILIPA DENI AKABAKI NA CHENJI……..

MAGWANDA YA SAULI (na silaha za vita) NA KOMBEO LA DAUDI

1 Samweli 17:49 Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi.

MWANZONI ALIJARIBISHA ASICHOKUWA NACHO….. 1 Samweli 17:38-39

Ndipo Sauli akamvika Daudi mavazi yake ya vita, akamtia chapeo cha shaba kichwani, akamvika dirii. Naye Daudi akajifunga upanga juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi akamwambia Sauli, Siwezi kwenda na vitu hivi, maana sikuvijaribu. Basi Daudi akavivua. USIFICHE KIPAWA ULICHONACHO KWA SABABU YA UNG’AVU KILE WALICHONACHO WENZAKO.. 

FIMBO YA MUSA

Kutoka 4:2 Bwana akamwambia, Ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, Ni fimbo. WAKATI UNAULIZA NANI ATANIPA KITU CHA KUNISAIDIA MUNGU ANAKUANGALIA NA HIYO FIMBO UNAYOIDHARAU…NDIYO YENYE MUUJIZA WAKO… SIYO KUCHUNGIA MBUZI TU… 

EE BWANA FUNGUA MACHO YANGU, NITAZAME NDANI YANGU, VITU ULIVYOWEKA NDANI YANGU NA KARIBU YANGU IKIWA NI PAMOJA NA MIKONONI MWANGU… NISAMEHE KWA KUVIDHARAU VINGINE NA KUTOTUMIA IPASAVYO.. NIPE NAMNA YA KUTUMIA…USHAURI WA KIUNGU KAMA ULIVYOMPA DAUDI NA KOMBEO LAKE, MAMA MJANE NA CHUPA YA MAFUTA, MJANE NA KONZI YA UNGA NA MAFUTA + WATOTO, FIMBO YA MUSA… NISAIDIE NIFUKUE NILIVYOFUKIA, NIVIPENDE NILIVYODHARAU, NISIMAMIE NILIZOTAWANYA…. KATIKA JINA LA YESU KRISTO

Mithali 17:8 Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; Kila kigeukapo hufanikiwa.

KIPAWA NILICHOPEWA NINAWEZA KUNIPA KILE AMBACHO NIMEKUWA NIKITESEKEA KWA MUDA MREFU

NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU 

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565

No comments:

Post a Comment