Wednesday, January 18, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 18

SIKU YA 18 - 18/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KULINDWA DHIDI YA MAGONJWA NA UDHAIFU WA KILA NAMNA

Kati ya mambo ambayo Yesu aliyabeba msalabani ni magonjwa na udhaifu wa kila namna, iliyokuwa imestahili kuwa yetu.

Isaya 53:5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu, Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona

Mathayo 8:17 .....Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.

Mathayo 4:23......na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna.

Magonjwa ya adui yasiwe juu yako ...

Yohana 10:10 ..Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; Mimi (Yesu) nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele

KILA UGONJWA NA UDHAIFU ULIO KWENYE MWILI WAKO SIO WA KWAKO NI WA ADUI, KEMEA KWA JINA LA YESU

OMBA..

YESU ALIKUJA ILI NIWE NA UZIMA TELE, NINAO UZIMA KATIKA JINA LA YESU, YESU ALIJITWIKA UDHAIFU WANGU, KATIKA JINA LA YESU.

MAGONJWA YA MLIPUKO YASINIPATE, KWA MAJINA YAKE. NIKO CHINI YA UVULI WA MWENYENZI MAGONJWA HAYATANIPATA...

Mwaka 2017 sitaangukia katika MAGONJWA ya aina yoyote..

SASA OMBA KWA MANENO YAKO* KAMA UNA udhaifu AU ugonjwa WA AINA Yoyote, OMBA Kemea

Mungu atakujalia utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment