Tuesday, January 17, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 16

SIKU YA 16 - 16/01/2017
Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA

KATAA UTASA/KUTOKUZAA KWENYE KILA KITU CHAKO

Kutoka 23:26 Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza.

SIYO KUSUDI LA MUNGU KUSHINDWA KUWA PRODUCTIVE/KUZAA KWANI AHADI YAKE KUTOKUWEPO MWENYE KUHARIBU MIMBA, TASA, WALA KUFA KABLA YA KUMALIZA HESABU ZA SIKU ZAKO…

Ayubu 3:7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe

SIKU ZA MTU ZINAWEZA KUFANYWA TASA.. UNAWEZA UKAWA UNAPIGA KAZI KWA BIDII LAKINI UKIFANYA EVALUATION NI KAMA ULIKUWA UNALALA TU NYUMBANI..

Ayubu 15:34 Kwa kuwa jamii ya hao wasiomcha Mungu watakuwa tasa, Na moto utateketeza mahema yenye rushwa.

KATI YA MAMBO YANAYOHARIBU NA KUFANYA WATU KUTOKUZAA NI KUTOMCHA MUNGU NA KUTOA RUSHWA/KUPENDELEA… KWANINI RUSHWA NI MBAYA?

Kumbukumbu la Torati 16:19 Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki. UWEZO WA KUFIKIRI KIMKAKATI KATIKA HAKI UNAPOTEA…

Zaburi 113:9 Huweka nyumbani mwanamke aliye tasa, Awe mama ya watoto mwenye furaha. LAKINI ASHUKURIWE MUNGU AJUAYE KUBADILISHA MAJIRA..ALIYE TASA AWE MAMA MWENYE FURAHA…

Mwanzo 25:21 Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba

UNAWEZA KUMWOMBA MUNGU AONDOE UTASA KWAKO NA MKEO (MUMEO) NA PIA KWENYE KILA JAMBO UNAOLIFANYA…

NATAMKA UZIMA JUU YA KILA JAMBO NINALOLIFANYA… HAPATAKUWA NA MWENYE KUHARIBU MIMBA, WALA ALIYE TASA, KATIKA NCHI YANGU; NA HESABU YA SIKU ZANGU BWANA ATAITIMIZA. SIISHI KATIKA RUSHWA NA UPENDELEO WALA KUTOA NA KUPOKEA RUSHWA… KUTOKUZAA, KUTOKUONGEZEKA HAITATAJWA KATIKA MAISHA YAKO KATIKA JINA LA YESU... KWA SABABU Mwanzo 1:28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.

NA IWE KWANGU KATIKA JINA LA YESU

MWAKA 2017 UZAO WAKO UONGEZEKE…. KAMA UNATAKA MTOTO UTAPATA MWAKA HUU

SASA OMBA KWA MANENO YAKO

KAMA UNA TATIZO LA KUTOKUZAA KWA MUDA MREFU OMBA HUKU UMEFUNGA NA USOME, 1 Samweli 1:1-28, Mwanzo 11:30, Zaburi 113:9, Luka 1:36-37

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment