Friday, January 13, 2017

2017 MWAKA WA KUTHIBITIKA - 13

SIKU YA 13 - 13/01/2017

Zaburi 40:2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.

KUWA ESTABLISHED/KUIMARISHWA/KUTHIBITIKA
KUSHINDA KUAMBATANA NA WATU WASIO SAHIHI/MAHUSIANO MABOVU

Mithali 7:7 Nikaona katikati ya wajinga, Nikamtambua miongoni mwa vijana, Kijana mmoja asiyekuwa na akili,

Sikutegemea kijana huyu awe na akili wakati yuko katikati ya wajinga…. Ndiyo maana ni vyema kumwomba Mungu akupe watu sahihi wa kuambatana nao… .SIMAANISHI WALIOKUZIDI TU BALI WANAOTAKIWA (RIGHT PEOPLE) Mithali 13:20 Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima; Bali rafiki wa wapumbavu ataumia

Changamoto ya kwanza ya Balaamu haikuwa uchawi wake bali watu waliombatana nao… ndiyo waliomshawishi awalaani Israeli…

MUNGU ANAMUULIZA BALAAMU Hesabu 22:9 Mungu akamjia Balaamu, akasema, Ni watu gani hawa ulio nao pamoja nawe?

MUNGU AKUFUNDISHE NA AKUSAIDIE KWA ROHO WAKE MTAKATIFU KUCHAGUA WATU SAHIHI MWAKA 2017

Wakati mwingine macho yanaweza kukudanganya ukaingia kichwa kichwa kumbe kuna hila kwa sababu umeangalia kwa nje tu…

KUNA MTU AKIFANYA “FRIENDSHIP ANALYSIS” UTAGUNDUA TANGU UANZE KUKAA NA BAADHI YA WATU UMEENDELEA AU UMERUDI NYUMA…. UNAONGEZEKA AU UNAPUNGUA… KIU YA KUMTAFUTA MUNGU INAZIDI AU INAPUNGUA… ANGALIA TABIA MPYA ULIYOIPATA… NZURI AU MBAYA???

1 Samweli 18:1 Ikawa Daudi alipokwisha kusema na Sauli, roho ya Yonathani, ikaambatana na roho ya Daudi, Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
MUNGU AKUKUTANISHE NA WATU SAHIHI WA KUAMBATANA NAO KATIKA JINA LA YESU

MWAKA 2017 UWE NA MAHUSIANO SAHIHI KATIKA JINA LA YESU….

SASA OMBA KWA MANENO YAKO

Mungu atakujalia hayo utakayoyaomba katika jina la Yesu

Apostle Shemeji Melayeki
GLOBAL FAMILY GATHERINGS MINISTRIES
PHONE: +255 714 548 565
We are the Standards! 2017

No comments:

Post a Comment