Friday, July 25, 2014

JE UMEKATALIWA

                 
 

Mara Nyingi utasikia mtu akisema yule jamaa Ana Roho ya kukataliwa au mimi jamani kila ninachokifanya nakataliwa au kila ninapoenda nakataliwa.                         
 
Inawezekana umekataliwa mambo mengi katika maisha tena kibaya zaidi umekataliwa na watu wako wa karibu kama ndugu, jamaa na marafiki au pia waweza.kujikuta umekataliwa na wafanyakazi wenzako au wafanyabiashara wenzako au watumishi wenzako, wanafanya maamuzi makubwa lakini hawakihusishi labda wanakudharau wanaona kwamba hustahili kujua.     
Mara nyingi familia zimekuwa na tabia ya kuwakataa na kuwatenga wenye kipato kidogo katika familia, yamkini wewe ni mzaliwa wa kwanza lakini familia haikudhamini IMEKUKATAA kwasababu hawaoni mchango wako na.kwakweli hujafanya makusudi ni kwamba huna tu cha kutoa, wameuza uzaliwa wako wa kwanza kwa mdogo wako ambaye ndio Tajiri wa familia, wanaamua maamuzi makubwa ya familia hawakushirikishi kwasababu tu huna kitu.     Ndugu yangu watu wamekudharau ,wamekucheka, wamekung'ong'a kwasababu huna kitu au huna elimu au huna mtoto au huna mwenzi wa maisha, labda hali yako ya kukataliwa imesababisha huna hata pa kukaa wala huna wa kukupa chakula Ndugu yangu nimekuja kuongea na wewe siku ya Leo waliokukataa ni wanadamu tu ila Mungu hajakukataa wala hana mpango wa kukutaa unayo sababu ya kufurahi siku ya Leo kwasababu mfalme wa wafalme ,Mungu Mkuu,Jehova,Yahweh,HAJAKUTAKAA.                 
 
Ukisoma 1 Petro 2: 4-9, utaona jinsi hata Yesu alikataliwa lakini maandiko yanasema katika mstari wa 4 "Mmwendee yeye jiwe lililo hai lililokatakiwa na wanadamu lakini kwa Mungu ni TEULE LENYE HESHIMA".                         
 
Yesu alikataliwa na wanadamu, alipigwa, alidhihakiwa, alitemewa mate,alidharauliwa , ALIKATALIWA tena kwa watu wake wenyewe wakimkejeli huyu si mtoto wa fundi seremala tu iweje Leo a anatuletea wokovu kwasababu wao walikuwa na madaraja kwamba labda katika ukoo Fulani tu au watu wa aina Fulani ndio tu wanaweza kuwa wazuri wakasahau Yuko Mungu ambaye njia zake hazichunguziki,anayejua Mwanzo na Mwisho wake, Leo ndugu yangu ukumbuke Mungu ni yeye yuleyule hajabadilika anakuon tofauti na watesi wako wanavyokuona, hali ya sasa isikufanye ukakata tamaa ukakosa Baraka na Miujiza Mikubwa iliyo mbele yako, hivi unajua ndugu yangu wewe ni Uzao mteule,kuhani wa kifalme, taifa takatifu, mtu wa Milki ya Mungu? Usisikilize kelele zao Mungu anakuwazia mawazo Mema, hakuna mwanadamu mwenye usemi wa mwisho juu ya mustakabali wako aliyekuumba ndio anajua mustakabali wako yeye ndio anakujua, wao wakiona maskini, Mungu anakuona Tajiri, wakikuona huzai Mungu anaona hakuna tasa katika Israel, wakiona wewe wa mwisho Mungu anakuona kichwa wala si mkia, Wewe ni Mshindiiii.                          
 
 Inuka Mungu HAJAKUKATAA.........Haleluyaa

Tuesday, July 22, 2014

TAMBUA BARAKA ZINAZOKUJIA ZINATOKA WAPI Sehemu ya Pili (II) na Mwalimu Samwel Mkumbo

Bwana Yesu asifiwe mpendwa wangu, Karibu tena katika makala haya ya mafundisho ya Neno la Mungu yanayoletwa kwenu na Mwalimu Samwel Mkumbo.
Kwa kifupi Mwalimu Samwel Mkumbo ni Mhitimu wa Chuo Kikuu mwenye wito na karama ya Kufundisha Neno la Mungu.

Karibu tuendelee na Sehemu ya Pili ya Somo hili lililoanza wiki iliyopita, kama hujasoma sehemu ya Kwanza nakushauri pitia katika blog hii usome sehemu ya kwanza ili kupata mtiririko mzuri wa Somo.

 
Mwalimu Samwel Mkumbo


Ø  Chanzo cha Mapato ya Anayetoa/ Chanzo cha Sadaka yenyewe.

Kuna wakati tunaweza kujua nini uamuzi wa kufanya au nini ni nia ya sadaka tunayopokea kwa kuangalia chanzo cha mapato ya anayetoa, au chanzo cha sadaka hiyo. Tazama mfano huu;

Huyo mfalme akawaagizia posho ya chakula cha mfalme,na ya  divai aliyokunywa, akaagiza walishwe hivyo muda wa miaka mitatu; ili kwamba hatimaye wasimame mbele ya mfalme……….. Lakini Danieli aliazimu moyoni mwake ya kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme, wala kwa divai aliyokunywa…….. (Danieli 1: 5, 8).

Ninachotaka tuone hapo ni kwamba pamoja ya kwamba hawa vijana watatu, naam, huyo Danieli, Meshaki, Shedraki na Abednego walipata nafasi ya kupata chakula kizuri kutoka katika meza ya mfalme tena wakiwa katika nchi ya ugeni bila kusahau walikuwa na hadhi ya utumwa, lakini hawakukubali kupokea hiyo Baraka au zawadi kutoka Ikulu, tena Biblia imeweka kweupe sababu yao, ni kwamba hawakutaka kujitia unajisi.

Maana walijua ya kuwa kuna uwezekano ya kuwa kama  ni nyama basi zitakuwa zilizokuwa zimetolewa sadaka kwa miungu ya Wababeli, lakini pia hawakupenda kunywa mvinyo yao wala kitu chochote, lakini pia hawakutaka kujitia unajisi kwa chakula cha mfalme na ilikuwa ni mila na desturi ya wayahudi kutoshiriki chakula na watu wa mataifa.

Japokuwa biblia haijaweka kweupe ni lini hasa au wakati ambao hao wakina Danieli waliacha kula mtama au ni lini walianza kula vyakula vya kawaida lakini sabab kubwa ya kukataa ni kwamba walikataa chanzo cha chakula hicho.

Ø  Uhusiano wa mtoaji na watu wengine.

Kuna wakati mwingine watu hupenda kuwafadhili watumishi wa Mungu na kuonesha wema kwa watumishi wa Mungu, tena sana. Lakini unakuta mtu huyo huyo huwatendea watu wa nyumbani mwake mambo maovu, na hata kama si watu wa nyumbani mwake lakini hata watu wengine wa kawaida huwatendea mambo yasiyo mema wala hawafadhili, au kuwatendea wema nga kidogo. Jambo kama hilo si jema na ni vema mtu kama huyo uwe nae makini sana maana inaweza kuwa mtego sana kwako, lakini pia inaweza kuwa laumu kwa hao anawatendea mabaya maana wanaweza kuona kuwa unawafanyia fitina,. Tusome pamoja hapa; 

……..Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio….(Wagalatia 6:10).

Lakini kwa makini tena tazama maneno haya…………tuwatendee watu wote mema;….na hasa jamaa ya waaminio…..

 

Ushauri wa Ziada.

Katika kukaa katika nafasi nzuri ya utumishi na mahusiano mazuri na watu na namna ya kuangalia jinsi tunavyotumika tazama kitabu cha TIMOTHEO.

Monday, July 21, 2014

The Assemblies of God to Celebrate 100th Anniversary in US





The Assemblies of God is the U.S.'s oldest Pentecostal denomination. (Assemblies of God)

Worldwide members of the Assemblies of God (AG), one of the fastest-growing international protestant denominations, will join together in the U.S. this fall to celebrate the AG's 100th anniversary year, the unity they have shared for the past century and the remarkable growth of the denomination globally.

Established as an outgrowth of the 1906 Azusa Street Revival among Pentecostals in the U.S., the General Council of the Assemblies of God was formed in Hot Springs, Arkansas, in April 1914 as a broad coalition of ministers who desired to work together to fulfill common objectives, such as sending missionaries around the world and providing fellowship and accountability.

"This centennial event will be a moment of revival, a moment of celebration and a moment of focusing on our mission, to complete the great unfinished task of ensuring every person has a chance to hear of Jesus' love for them," said Dr. George O. Wood, General Superintendent of the Assemblies of God. "This 100th anniversary gives us the opportunity to focus on what God still has for us to do as we look with joy to our past history, give thanks for the present and look forward to what we still have to accomplish in the future."

Following its formation in 1914, the Assemblies of God quickly took root in other countries and formed indigenous national organizations. The Assemblies of God throughout the world now exceeds 67.5 million adherents, including more than 3.1 million members in the U.S. The denomination has experienced 24 years of consecutive growth, bucking the trend among most other U.S. denominations in recent years.

The Centennial Celebration will be a truly international event, with guest speakers from AG churches all over the world. In addition to Dr. Wood, keynote addresses will be delivered by Yong Mok Cho of South Korea, Juan Carlos Escobar of Spain, Edward A. Grabovenko of Russia, Lazarus Chakwera of Malawi, Barnabas Mtokambali of Tanzania, Ivan Satyavrata of India, José Wellington of Brazil and Max Schläpfer of Switzerland. Other U.S. speakers include Hal Donaldson, John Lindell, Wilfredo "Choco" De Jesús, Nam Soo Kim, Jason Frenn (who ministers in Latin America) and Raegan Glugosh, a U.S. missionary to Romania.

The Centennial Celebration is expected to be one of the largest international gatherings of AG members, with more than 5,000 individuals traveling from 112 different countries to attend.

In addition, many of the sessions will be carried live via direct simulcast and international television networks. Churches throughout the U.S. will serve as live simulcast hosts, while Unsión will broadcast live to Latin America, where the AG has over 30 million adherents, and LMTV will broadcast live to Africa, where the AG has over 17 million adherents.


Source: Charisma
 

Tuesday, July 15, 2014

TAMBUA BARAKA ZINAZOKUJIA ZINATOKA WAPI na Mwalimu Samwel Mkumbo

Bwana Yesu asifiwe mpendwa karibu sana katika makala haya yanayoletwa kwenu na Mwalimu Samwel Mkumbo.

Mwalimu Samwel Mkumbo
Hakika Baraka ni jambo mojawapo la msingi sana kwa  watoto wa Mungu na ni jambo la Faraja tuonapo mwana wa Mungu akifanikiwa katika mambo yake yote. Kama inenwavyo;

..,….Mzee, kwa Gayo mpenzi, nimpendaye katika kweli. Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo…,… (3Yoh 1:1-2)

Sasa basi ni vema ukafahamu  ya kuwa kubarikiwa ni jambo la msingi sana na tena ni moja ya ushuhuda kwa watoto wa Mungu. Lakini pia Baraka ni kutukuka sana katika Ukuu wa Mungu na pia juu ya haya yote tunaweza kuona ni kwa jinsi gani uweza  wa Mungu unajidhihirisha katika mambo yetu ya mwilini naam katika kutuma mema katika Tumaini jipya la imani yetu.

Lakini pia Biblia inatupa maelezo kadhaa juu ya kupata Baraka au mafanikio maana si kila mafanikio (Baraka) zina mkono wa Mungu ndani yake, au ni utukufu wa Mungu mingine ni mitego ya shetani katika kutuangusha katika imani yetu katika KRISTO YESU, naam! Maandiko matakatifu yanatupa mifano kadhaa ya Baraka zitokazo kwa Mungu na zile zinazoletwa na mwovu kama mtego kwetu.

Vielelezo!!

-Habari za Elisha na Naamani.

2 Wafalme 5:1-14 tunaona kisa kizuri na cha kutufundisha juu ya Baraka.

Nabii Elisha alipata nafasi ya kufanya muujiza wa uponyaji kwa Naamani (Yule jemadari wa Shamu) juu ya ukoma wake, na baada ya muujiza huo, mtu huyo, huyo Naamani alitaka kumpa zawadi Elisha, lakini Elisha hakukubali,. 2 Wafalme 5: 15-16 inasema;

Akamrudia Yule mtu wa Mungu, yeye na mafuatano yake yote. Akaja, akasimama mbele yake; akasema, Sasa  tazama, najua ya kwamba hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli; basi nakuomba upokee mbaraka kwa mtumwa wako. Lakini akasema, Kama BWANA aishivyo ambaye nimesimama mbele yake, sipokei kitu. Akamshurutisha apokee, lakini akakataa.

Katika maandiko hayo utaona ya kuwa Elisha hakupokea Baraka kutoka kwa Yule Jemadari naam, huyo  Naamani, lakini ni vema tukafahamu ya kuwa si kwa sababu Elisha alikuwa na tabia ya kutopokea zawadi na Mbaraka kutoka kwa watu aliowahudumia, la hasha! Bali ipo sababu nyingine, maana  ni Elisha huyu huyu alipokea msaada kutoka kwa mama Mshunami! Tazama hapa;  2Wafalme 4:8

Kwa hiyo si kila tunuku unayopewa ni ya kukubali lakini pia si zote ni za kukataa maana kila jambo lina maana yake na matokeo yake ambayo kwa hayo twaweza kutambua kusudi na mapenzi ya Mungu kwetu lakini pia hila na mitego ya shetani.


-Mfano wa Yesu.

Wednesday, July 2, 2014

Nigerian Gospel Singer Sinach weds Pastor Joseph

 
Nigeria Gospel Singer, Osinachi Kalu popularly known as Sinach last Saturday June 28th exchanged vows with Pastor Joseph at Christ Embassy Church, Ikeja, Lagos.
 
Sinach is Globally known for her  hit Song " I Stand Amazed"
 
 
Sinach and Husband Pastor Joseph
 
 
With this Ring....
 









 


Wow I am so happy for you Sinach