Monday, June 23, 2014

NAFSI ILIYONASWA na UZINZI na Frank Philip



Mtumishi Frank Philip
Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani …Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake. Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika” (Mithali 6:26 & 32,33).

Nimeona jambo hili, nami nikatafuta kujua kama kuna hekima ndani yake “men’s hearts can be shared, but women’s hearts replaces”. Maana yake: Moyo wa mwanaume ukipenda, waweza kupenda tena kwa wakati mmoja, ila moyo wa manamke ukipenda, humwondoa wa kwanza na kumpenda mwingine.

Ukitaka kuona kwa njia ya urahisi, jiulize ni kwanini mwanaume mmoja anaweza kuoa wake zaidi ya mmoja na maisha yakaenda? Na jiulize tena, je! Mwanamke anaweza kuwa na mpenzi wa nje ampendaye sana, na maisha yake ya ndoa/mahusiano yakawa sawa? Wote wawili: mwanamke na mwanaume, wana hatari ya kuingiliwa mioyoni mwao, japo kwa madhara tofauti.

Hii hali sio rahisi kuikubali katika mahusiano ya kawaida ambapo mtu anatoka nje ya ndoa/uhusiano kwa siri. Mara nyingi mtu afanyaye mambo hayo, hudhani yuko sawa, kumbe ameathirika kabisa. Ukitaka kujua ninachosema, angalia mambo ya kawaida kabisa ya kwenye ndoa/uhusiano kwa watu ambao mmoja au wote wamenaswa nafsi na kahaba. Mambo ya kawaida kabisa kwenye uhusiano/ndoa yanaanza kuwa kero, mzigo na ya kuchosha. Ukiona hii shida, usipambane na mtu kwa jinsi ya mwilini, shughulika na nafsi kwa sababu hapo ndipo penye shida.

Nitasema na wanawake sasa. Hii hali ya “replacement”, huwa haianzi mara moja. Huenda kwa awamu, na hatua mbali mbali, kuanzia hisia, matendo kisha ngono. Ndio maana mwanamke akitoka nje ya ndoa watu husema “amefika mbali”. Mara zote huanza na “nafsi kunaswa” na kahaba. Kama kuna mtego mbaya, ni kuacha nafsi yako inaswe. Kwenye nafsi ndiko kuliko na mawazo na maamuzi. Kama nafsi imenaswa, mara ZOTE mtu ataanza kuwaza tofauti, na kisha kufanya maamuzi mabaya. Ndio maana tunaonywa sana kwamba “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima” (Mithali 4:23). Ukitaka kuona uzima kwenye ndoa/uhusiano wako, linda sana moyo wako; ukitaka kuona mauti kwenye ndoa/uhusiano wako, achilia moyo wako uingiliwe.

Friday, June 20, 2014

Mwimbaji wa Nyimbo za Injili na Mama Mchungaji Deborah Said amefariki Dunia

 
Deborah Said wakati wa uhai wake
 
Mama Mchungaji na mwimbaji wa Nyimbo za Injili Debora Said amefariki dunia usiku wa kuamkia leo tarehe 20/06/ 2014 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili

Deborah Said ni mke wa Mchungaji John Said wa Kanisa la Victorious Living lililopo Mabibo External

Marehemu ameacha watoto wanne na Mgane Mchungaji John Said

Katika Uhai wake Deborah Said alikuwa ameimba nyimbo mbalimbali za Kumsifu na Kumwinua Mungu, utumishi wake uliwagusa wengi hata Tanzania, siku si nyingi alikuwa amezindua albamu yake ya Mti wenye Matuda

Deborah Said akizindua Albamu yake ya Mti wenye Matunda kabla hajatangulia kwa Baba
 
Blog imefanikiwa kuongea na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili wa Chama  cha Muziki wa Injili Tanzania  MC Joshua Makondeko ambaye amesikitishwa sana na msiba huu na Mara nyingi tuliona akituomba sana katika facebook wall yake tumuombee Deborah na hata Deborah aliporuhusiwa hospitali  aliendelea kumshukuru Mungu kwa Uponyaji wa mwimbaji huyo wa nyimbo za Injili, kwasasa MC Joshua Makondeko yuko safarini  Rukwa ameomba kila waimbaji wa Injili wote wafike kuifariji familia pia wafike na mchango wa elfu 10 wamuone Cosmas Chidumule

Msiba uko nyumbani kwao nyuma ya Mabibo Hostel karibu na Pepsi Bar uliza kwenye Msiba wa mama Mchungaji

Programu ya mazishi itakuwa kuanzia hawajaamua mpaka sasa ila itakuwa kuanzia wiki ijayo, Blog itaendelea kuwapata taharifa ya Ratiba ya Mazishi


POLENI WOTE KWA MSIBA HUU,Roho Mtakatifu Awafariji yeye ndiye Mfafiji wa Kweli
 

Thursday, June 19, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Jiepushe na Mahusiano ya Zamani


 
Bwana Asifiwe wapendwa karibu tena katika Masomo yenu ya Uchumba hadi Ndoa yanatoletwa kwenu na Mshauri wako.

Leo tutazungumzia jambo muhimu sana ambalo limesumbua mahusiano mengi ya uchumba na Ndoa pia, jambo lenyewe ni Mahusiano ya nyuma ambayo mtu alikuwa nayo. Mahusiano hayo ni kama mkaka au mdada alishakuwa na mchumba mwingine huko nyuma lakini ikashindikana kuendeleza mahusiano ikabidi wavunje uhusiano. Hayo ndio mahusiano hasa nitakayozungumzia leo.

Mahusiano ya nyuma mara nyingi huvunjika pale mnaposhindwana tabia, mitazamo, maamuzi na kadhalika na kadhalika.

Mpendwa wangu yamkini huko nyuma kabla ya kukutana na huyo mtarajiwa wako ulishakuwa na Mahusiano, ni muhimu sana kuhakikisha unachukua maamuzi thabiti kuhakikisha kwamba hayo mahusiano ya nyuma yanaisha na hakuna kingine kinaendelea kati yenu zaidi ya salamu tena tu ikitokea tu mmekutana uso kwa uso sio unaanza kumpigia simu enhee unaendeleaje hiyo ni hatari na dhambi ya kutokuwa muaminifu. 

Siku hizi ndoa zina shida kubwa ya Cheating kwasababu watu hawakuachilia mahusiano ya nyuma. Au unakuta mtu anampigia Simu yule mwenzi wa zamani na kumuelezea jinsi anavyopata matatizo labda na uhusiano wa sasa wenyewe wanaita a sholder to cry.

Nasikitika sana maana hayo mambo yako makanisani pia siku hizi ni jambo la hatari sanaaa.     Sasa wengine wataendeleza huo uhusiano kwa siri mpaka wanafunga Ndoa unaendelea hivyo hivyo kwahiyo utashangaa Ndoa mwezi imevunjika kumbe shida ni Mahusiano ya Zamani jamani hiyo Roho ishindwe naikemea kwa Jina la Yesu.

Nilisoma mahali kuna dada alikuwa anakwenda kuolewa ile siku moja kabla ya ndoa eti akaenda kuagana na mtu wake wa zamani basi yaliyomkuta huko ikawa ni mauti na dunia nzima kujua siri na uchafu huo alikuwa anaufanya.

Unaweza kuona labda leo hujakamatwa lakini unatakiwa ujue mpendwa wangu Mungu hapendi vuguvugu kama umeamua mimi ni wa Yesu mfuate umeamua kurudi nyuma kaa nyuma lakini usijifishe kanisani ukajifanya kondoo kumbe wewe ni mbwa mwitu unamfanyia mwenzako ubaya anakuamini sana anafikiri amepata mwenzi mwaminifu kumbe wewe unafanya uasherati ndugu kuna malipo, Jihadhari ndugu yangu.

Mahusiano ya zamani ndio chanzo cha nyumba ndogo tunachoona katika jamii watu wamegeuza fashion.. Siku hizi mtu haogopi kama huyo mtu ameoa au ameolewa ni Hatari mpendwa Jihadhariii.

Madhara ya Mahusiano ya Zamani:      

Tuesday, June 17, 2014

KKKT Kinyerezi: Watu wasiopungua 50 wampa Yesu maisha yao katika Ibada ambayo Mwalimu Samwel Mkumbo alihudumu

 
Mwalimu Samwel Mkumbo akifundisha Neno la Mungu katika Kanisa la KKKT Kinyerezi
 
Watu wakisikiliza neno la MUNGU kwa umakini

Kwaya ya vijana Mwenge KKKT wakiimba

Mwalimu Mkumbo akifundisha na kusisitiza jambo

Watu wasiopungua hamsini walimpa Yesu maisha yao, Utukufu kwa Bwana Yesu
 
Watu wakishangilia baada ya kumpa Yesu maisha yao, Halleluya

Maombi yakiendelea, kuombea pia kamati mbalimbali za Kanisa
 

                                 Mch. Manford akiwa na Mwl Samwel Mkumbo
 
 
 

Thursday, June 12, 2014

World Cup 2014: Bibles being distributed to thousands



International outreach organization the Bible Society will minister to thousands, if not millions, this week in Brazil during the FIFA World Cup.

Through the organization's Joga Limpo Brasil movement (Fair Play Brazil), the Bible Society of Brazil will distribute four million pocket-sized Bibles, 20,000 copies of the Gospel of John in nine different languages, and World Cup editions of the New Testament and the Bible.

Over half a million soccer fans are expected to flock to Brazil this week for the world's most popular sporting event, and there are millions of Brazilians expected to attend the games. Rev Dr Rudi Zimmer of the Bible Society of Brazil described the excitement in the country surrounding the games, and his motivation for embarking on the huge outreach campaign.

"Brazilians are football-mad and their obsession with football will reach fever pitch over the next few weeks, when we host the World Cup," he said in a press release

Tuesday, June 10, 2014

COME AND DRINK By Pastor Malonga


Pastor Malonga
Opening Scripture John 7:37-39
37 On the last and greatest day of the festival, Jesus stood and said in a loud voice, “Let anyone who is thirsty come to me and drink. 38 Whoever believes in me, as Scripture has said, rivers of living water will flow from within them.”[a] 39 By this he meant the Spirit, whom those who believed in him were later to receive. Up to that time the Spirit had not been given, since Jesus had not yet been glorified.

 

Man composed of three parts;

1.      Body

Outer physical part

You can touch it

You can see with physical eyes

You can feel it

 

2.      Spirit and Soul

Invisible

They work together

You cannot separate them

 

Body will die and separated from Spirit and Soul, but Spirit and Soul cannot be separated they can go together in hell or heaven

 

Our Physical body need water to survive, without water it will dehydrate then die

God has placed in-built sensors in our body when body get dehydrated sensors will send information that there is no water

Just as body needs water for its sustenance similarly Spirit needs Spiritual water for its survival

The Spiritual water is the Holy Spirit

In Verse 37  it says On the last and greatest day of the festival, Jesus stood and said in a loud voice, “Let anyone who is thirsty come to me and drink

Jesus shouted meaning this was an important announcement

Most of us are concentrating on outer man and disregarding the inner man

Feeding and ensuring it looks nice

But I want to tell you today the outer man is temporary but inner man will live forever

Thursday, June 5, 2014

KIVULI cha NAKALA HALISI na Mwalimu Frank Philip

Karibu katika makala haya ya Mafundisho ya Neno la Mungu yanayoletwa kwenu na Mtumishi wa Mungu Frank Philip.


Mwalimu Frank Philip
Katika maisha ya kila siku, tumekuwa na utaratibu wa kutumia KIVULI (copy) cha nakala HALISI (original), kwa matumizi mbali mbali. Mara nyingi, kama sio zote, kivuli cha nakala halisi huweza kutumika kama nakala halisi, hadi kuwe na ulazima wa kuonesha nakala halisi. Kwa mahali pengine, kivuli cha nakala halisi hakiwezi kusaidia kitu, hadi nakala halisi iwepo. Kwa matumizi ya kuanzia (preliminary use), kivuli cha nakala, huwa ni kitu cha msaada; kwa matumizi mengine maalum, kivuli hakimfai mtu kitu. Kwa mfano, huwezi kusafiri na kuingia nchi nyingine kwa kutumia vivuli vya nyaraka za kusafiria. Ndiyo ilivyo hata kwa nchi tunayoiendea baada ya maisha haya, jina lake ni Yerusalem mpya, ushukao kutoka juu. Huwezi kuingia na kivuli cha wokovu, unahitaji vazi halisi. Wokovu ni vazi jeupe, limeoshwa kwa Damu ya Mwana-kondoo. Huwezi kuingia kwenye karamu ya Mwana-kondoo bila vazi halisi.

Sifa moja kubwa ya kivuli cha nakala halisi ni kufanana sana, hasa kwa kubeba taarifa muhimu. Mara nyingi, kama sio zote, kulingana na kinakilishi (photo copier), ni vigumu kubainisha kati ya kivuli na halisi, hadi kwa kutumia vifaa maalum (counterfeit detectors). Bwana Yesu akasema, “acheni msing’oe, msije mkang’oa na ngano pia”! Hii inaonesha mfanano wa hali ya juu kiasi kwamba unaweza kung’oa ngano ukidhani ni gugu. Hivi ndivyo ilivyo hata kwa watu wenye majina ya kuwa hai, kumbe! Wamekufa. Tunadhani tuko na wenzetu, kumbe ni kivuli tu! Dhambi huleta mauti. Atendaye dhambi ni wa Ibilisi, japo anaishi, amekufa. Kweli hatuokolewi kwa matendo ya sharia, ila matendo yako yatakufanya kuwa kivuli au halisi.

Kwa kuelezea jambo hili, Bwana Yesu alitumia mfano wa magugu na ngano (Mathayo 13:24-30). Kwa bahati mbaya, kila shamba la ngano huwa na magugu, tena mengi. Ndipo wanafunzi wake waliposhangaa, kwanini Bwana hakutoa kibali cha kung’oa magugu mara moja? Bwana Yesu alisema “acheni magugu na ngano vikue pamoja”. Angalia neno hili, wakati ngano inakua, na magugu yanakua pia. Laiti kimoja kingekua zaidi ya kingine, ndipo tofauti ingekuwa dhahiri. Lakini ona sasa, kila ngano ikuapo, magugu hukua pia!

Nikitizama mfano wa magugu na ngano najifunza mambo mengi. Kwanza, magugu na ngano yanaweza kuwa kiwakilishi cha jamii ambayo hapa naita “shambani mwa Bwana”, kwa lugha nyepesi, mkusanyiko wa waaminio. Sasa najua shambani mwa bwana ni zaidi ya mkusanyiko wa waaminio, lakini kwa sasa, nachukua kundi la wana wa Mungu kama ngano, na kundi la wana wa giza kama magugu. Ona jambo hili, wote wanakaa katika shamba moja; na Bwana anasema, usiwatenganishe, waache wakue pamoja! Pili, nikaona jambo hili kuwa la msingi sana, Je! Kama ngano ingetengwa kabisa na magugu, tungejuaje sifa za ngano fulani katika kupambana na mazingira yake? Nani angejua tofauti ya ngano bora na mbovu, dhaifu na njema? Kwa maana, kama ngano ikizidiwa na magugu, basi kila mmoja atajua udhaifu wake. Kumbuka imeandikwa “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo” (Ufunuo 21:17). Lakini kukiwepo na ngano ambayo itastahimili magugu, na kuzaa kati ya magugu hayo, na kuonekana kwa dhahiri tofauti yake baina ya magugu, hiyo itakuwa ngano njema na yakusifiwa. Naam, yafaa kutunzwa ghalani, kwa maana ni ngano njema. Kwa ngano dhaifu, mara ipandwapo, hukua ila ilitingwa sana na magugu, na yamkini kushindwa kuzaa, na hatimaye kufanana na magugu kabisa. Ngano dhaifu namna hii, isiyozaa, haina tofauti na gugu, kwa maana imefanana sana, japo kwa jina, inaitwa ngano, hiyo ni gugu tu.

Tuesday, June 3, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Sababu Kumi zinazofaa kumfanya mtu aamue Kuoa au Kuolewa


Karibu tena katika Makala haya yanayoletwa kwenu na Mshauri wako wa Ndoa na Mahusiano, Leo tunaendelea na Sababu Kumi zinazofaa kumfanya mtu aamue kuoa au kuolewa , tukimalizia sababu tano zilizobaki
 
Tuendelee

 

6.      Kuambatana na Urafiki kweli

Lengo kubwa la Ndoa ni wanandoa kuwa na mahusiano ya yaliyojengwa ndani ya urafiki na kuambatana

Rafiki ni mtu ambaye mnashirikiana katika mambo mengi, ni mtu unayependa kumuona na kuzungumza naye mambo yako, ni mtu ambaye ukiwa na huzuni utapenda awe wa kwanza kumwambia, ukiwa na furaha pia utamshirikisha furaha yako. Hata ikitokea mmetofautiana na kugombana na rafiki hutajisikia vizuri utatamani tu utafute njia ya kutatua mgogoro na urafiki uendelee.

Na marafiki wengi wa kweli ambao wamekuwa marafiki wa muda mrefu wamepita katika vipindi vingi, kuna kipindi wamegombana, wamekwazana na wamefurahi sana kwa pamoja lakini wameendelea kuchukuliana na dio maana urafiki wao unaendelea.

Hivyohivyo ndoa inapaswa kujegwa katika urafiki wa dhati na wa kweli, ili kuweza kuchukuliana pale mnapopishana

Kwahiyo ukitaka kuingia katika ndoa uwe Tayari kumfanya mwezi wako kuwa Rafiki hapo utafurahi sana katika ndoa, maana utakuwa huru kwa mwenzako, kumtania, kumweleza chochote, na hata kama hujafurahi utamwambia nay eye pia, na pale mnapokwazana kwasababu ni rafiki itakuwa rahisi sana kusulihisha mgogoro. Kwahiyo kijana na binti yangu ingia katika ndoa na mtazamo huu utakusaidia sana

Usije ukamfanya mwenzako baba au mama yako, mama na baba wana nafasi zao tunaziheshimu, mfanye mwezi wako kuwa rafiki, Haleluyaaaaaaaaaaaa

 

Hata Neno katika Mwanzo 2 : 21- 24 “Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,

na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.

Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.”

 

Mungu aliona ni vyema wana ndoa kuwa Mwili mmoja na kuambatana, hamwezi kuambatana pia kama sio marafiki ndio maana leo tumeona ndoa nyingi wameshindwa kuambata kwasababu mahusiano yao hayana urafiki, Mungu akusaidie wewe unayetegemea kuingia katika ndoa ujifunze hili na wewe uliyeko katika Ndoa basi anza leo kuwa na urafiki na mwezi wako ili muweze kuambatana, yaani mkifanya mambo yenu kwa pamoja

 

7.      Ushirika

Ndoa ni nafasi nzuri sana ya kuweka ushirika katika matendo,yamkini umelelewa katika mazingira ya ubinafsi mpendwa wangu ambapo chako ni chako, hakuna mtu anavaa hata ndala zako, au hata anayegusa kitu chako, sasa ukiingia katika ndoa ujue mambo yatakuwa tofauti, kama Neno la Mwanzo 2: 21-24 Ndoa ni kuambatana inabidi ufungue moyo wako kuwa Tayari kushirikiana na mwenzi wako katika mambo yote, katika huzuni, changamoto, hali ya kupungukiwa, furaha na raha, sio kwa vile leo umeolewa na mwenzako anavitu basi unashirikiana naye akiishiwa tu au wanavyosema wana dotcom akifulia unamkimbia si sawa, hiyo sio ndoa mpendwa. Jiweke Tayari kushirikiana na mwenzako hapo utaona maisha mazuri utakuwa unaimba haleluyaaaa

 

8.      Kusaidiana mahitaji ya kila mmoja

Monday, June 2, 2014

Kenyan Christian leaders oppose polygamy bill


Christian leaders are appealing to President Uhuru Kenyatta not to sign into law a proposed new marriage bill that legalizes polygamy.

 (Date unknown) A Christian wedding in the Wakamba native reserve near Nairobi, Kenya, which was held in a mission church in the reserve. Religion News Service file photo 

Legislators passed the law last week after an intense debate that saw women members of Parliament storm out in protest. The bill’s passage followed an amendment to the existing marriage legislation to allow men to marry as many women as they want. It awaits Kenyatta’s signature to become law.

But the National Council of Churches of Kenya, the Kenya Conference of Catholic Bishops and the Evangelical Alliance of Kenya, have rejected it, saying the law will undermine Christian principles of marriage and family.

The Rev. Peter Karanja, general secretary the Kenyan church council, said the bill demeans women and fails to respect the principle of spouses’ equality in marriage.