Wednesday, May 14, 2014

Uchumba hadi Ndoa: Usioe au Kuolewa kwa msukumo wa Sababu hizi kumi zisizofaa


 
Habari mpendwa wangu, Karibu tena wiki hii nyingine nzuri Mungu ametupa tuzungumze na kushauriana

Leo tunaendelea na somo letu zuri tuliloanza wiki iliyopita la Usioe au Usiolewe kwa Msukumo wa Sababu hizi Kumi zisizofaa

Halleluya nasikia furaha sana kupata kibali cha kuzungumza na wewe siku ya leo.

 

Haya tuendelee na zile sababu tano zingine;

 

6.      Hofu ya kujitegemea

Kuna watu wengine ni tegemezi sana kwa wazazi wao,utegemezi huu unaweza ukawa umesababishwa na malezi wazazi waliwalea au yeye mwenyewe tu ni mvivu.

Utakuta mzazi anamfanyia mtoto kila kitu, atamtafutia chuo, atampeleka chuo, atamtafutia kazi, atamtafutia kiwanja,kupikiwa, kufuliwa etc,yaani mtoto anafanyiwa kila kitu kiasi kwamba yeye mwenyewe hana nafasi ya kuwaza na kufanya vitu peke yake. Sasa hapo pia inategemea na mtoto mwenyewe kama anapenda hiyo hali ndio atabweteka hivyohivyo.

Sasa basi akiona amekaa kwao na umri unaenda sana na wazazi labda wanamshauri apange nyumba na kujitegemea yeye anapata woga kwasababu alizoea kufanyiwa kila kitu ili kukwepa hayo anaamua aolewe au aoe na yeyote anayejitokeza ili tu apate pa kutegemea.

Sasa ndugu yangu kama umemuoa mtu au umeolewa na mtu kwasababu ya huo woga unafikiri kweli utaiweza ndoa, na je huyo uliyemtegemea akashindwa kufikia hayo matarajio yako ya utegemezi si utakimbia, nakuomba leo badili mtazamo usichukua uamuzi wa kuingia kwenye ndoa kama sehemu ya kumtegemea mwenzio akufanyie fanyie, badilika leo ndugu yangu, kuolewa ni kuzuri pale tu panapofanyika vile Mungu anataka na kama nilivyosema mwanzo kuna sababu nzuri tu za kuoa au kuolewa lakini sio hofu ya kujitegemea.

 

7.      Hofu ya kumuumiza mwenzako

 

Inawezekana ulikuwa kwenye mahusiano ya uchumba, lakini muda ulivyoendelea ukaona kwamba huwezi tena kuendelea na huo uhusiano inawezekana kwa sababu nzuri tu

Sasa labda ukiangalia muda ambao mlikaa katika huo uhusiano, mambo mliyoahidiana na kufanya pamoja, labda jinsi jamii inavyowatambua, ukaingiwa na hofu kwamba kwakweli sitaweza kumwambia huyu kaka au dada kwamba siwezi kumuoa au kuolewa naye kwasababu nitamuumiza sana. Matokeo yake unamuoa au unaolewa na mtu ambaye kiukweli hukupenda ila ni kwasababu uliogopa kumuumiza.

Sasa vile vitu vilivyokusababisha utake kufanya uamuzi wa kuachana nae na wewe ukashindwa kwasababu uliogopa kumuumiza, ujue kwenye Ndoa ndio utaviona vizuri sana tena clear, sasa sijui utamlaumu nani unaanza kukosa raha na mwisho kama hutakuwa makini na Mungu kuingilia kati hiyo ndoa inaweza kuvunjika kabisaa.

Au mwingine anaamua kabisa kumwambia mwenzake kwamba kutokana na jinsi huu uhusiano unavyoenda naona tuvunje kabla hatujaenda kupata matatizo katika ndoa, sasa mwingine hasa wakina dada Analia hapo mawiki na mawiki, na mwingine anatishia kujiua, sasa mkaka akiona hivyo anaogopa kwamba mwenzake atapoteza maisha kwasababu yake kwahiyo analazimika kuendelea na mahusiano hadi ndoa.

Je unategemea akimuoa huyo aliyetishia kujiua na bado ulikuwa na sababu za msingi za kuvunja uhusiano unafikiri maisha ya ndoa yatakuwaje? Hebu tafakari

Nakumbuka kuna kijana aliniambiaga namuoa fulani kwasababu unajua nimekaa nae miaka mingi sasa nimempotezea muda japo simpendi lakini namuonea Huruma,hiyo si sawa bora uchumba uvunjike kwa machozi kuliko Ndoa jamani naomba kusisitiza, Haleluya bado unanipenda jamani maana kuna watu wanapenda kung`ang`ania wee kama kakukataa jamani sio mwisho wa Safari na wala hutakufa kwa kumkosa tena baadae ukijam kutafakari  kwanini nilikuwa napoteza muda kwa mtu kama huyu utajicheka sanaaaaa cause they don’t deserve you, Wewe ni mtoto wa Mfalme Bwana, Ambassador of Christ why worries enhee! Aminaaaa!

 


8.      Kuwa mshauri wa Mtu

Yamkini kuna mkaka au mdada akakushirikisha machungu anayopitia katika mambo ya mahusiano, tena nimegundua ni strategy watu wanatumia siku hizi anakwenda kumweleza mtu mambo anapitia katika mahusiano anajiliza weee huko kumbe anataka awe na mahusiano naye. Jamani tuwe makini shetani kila siku naye anatunga mbinu mpya kama Teknologia inavyobadilika nay eye anabadili mbinu hivyohivyo.

Sasa wewe mkaka mdada kaja na kilio kwamba amepata mateso katika mahusiano yake ya huko nyuma, labda alibakwa, au alifanyiwa unyama mbalimbali, kwakweli hivyo vitu vikakuumiza ukaona mmh huyu kwasababu amenishirikisha acha tu nimuoe ili niwe namsaidia kumshauri, Kuwa makini kama hiyo tu ndio inakusukuma kumuoa ujue maisha ya Ndoa ni ya milele kifo tu ndio kitawatenganisha sasa kama utakuwa uliamua juu juu itakugharimu sana ndugu yangu.

Wewe kama ni mshauri fanya kazi yako ya ushauri na muombee lakini uwe makini na maamuzi yanahusu mahusiano na huyo mpenda, uwe na uhakika kwamba ni mpango wa Mungu na sio msisimko wako au Huruma yako inakufanya umuoea, Halleluyaaaa

 

9.      Kufanya Tendo la Ndoa kabla ya Ndoa

Inawezekana mmekuwa kwenye uchumba mkaanguka na kufanya tendo la Ndoa,

Tendo la Ndoa ni kwa ajili ya Ndoa tu na si vinginevyo, ndivyo Mungu aliweka. Sasa basi kama mtu amejikuta kaanguka basi ATUBU haraka sana na kuacha. Halleluya, na Ujue Mungu ni mwaminifu atakusamehe. Hapo utakuwa na kazi pia ya kujisamehe mwenyewe ama sivyo hiyo hali itakusumbua sana katika Ndoa.

Kama wachumba au watu wako katika mahusiano wakaanguka na kufanya tendo la Ndoa na baadae mmoja akaona kwamba kuna tabia au vitu vitamfanya avunje mahusiano, Hapo ndio inakuwaga shughuli sana hasa kwa wadada wengine utakuta wanang`ang`ania lazima unioe kwasababu umeniharibia usichana wangu kwahiyo mkaka atakuwa tu kalazimishwa kuoa huyo dada labda kwa Huruma na vitisho lakini zile tabia alizokuwa nazo mwanzoni kumbuka kwamba hazitabadilika tu kwa sababu tu amekuoa au umemuoa zitakuwa palepale. Hiki kinaweza kusababisha matatizo makubwa katika Ndoa na hadi kusababisha kuvunjika, kwahiyo mpendwa unavyomng`ang`ania huyo kaka au dada kuwa makini sana ni NINI MSUKUMO wako ? Mungu anasemaje katika Hilo? Unajua kama ni aibu Mungu amesemaje jamani Tumpe yeye aibu zetu zoote sio moja nay eye atatusitiri na ndio maana yeye ni Mungu Mkuu. Sasa kung`ang`aniza ndoa ili ufiche aibu mmh si sawa…Helooo

 

10.  Kupata Ujauzito

 

Haya mdada umekuwa na mahusiano huko na mtu ambaye labda kila siku anakupa presha, leo yuko na Jane, kesho yuko na Pendo, leo Lilian ,kesho Clara then jana Manka, wewe sasa kwasababu unajua kupenda mpaka hujitazami mwenyewe unang`ang`ania na sasa kwasababu ameshajua wewe ndio umefika atakuambia chochote na hadi atakushawishi mfanye tendo la ndoa kabla ya ndoa na wewe ukakubali, halafu baadae ukapata ujauzito, sasa wewe kwasababu ya ule ujauzito na unajua wazazi wako walivyo wa Kiroho na hawapendi hiyo mambo umefanya unamng`ang`aniza huyo jamaa akuoe tena kwa vitisho nitakunywa sumu, ooh nitakulaani nakadhalika nakadhalika, sasa wewe unafikiri akishakuoa ndio atabadilika na ile style yake ya kuchange wadada ujue ataendelea hivyohivyo sasa unaaza kujuta, na usipokuwa makini ndoa itakuwa Ngumu kama sio kuvunjika kabisa.

Kwakweli single parenting inauma lakini ni bora tu Utubu kwa Mungu wako ulee mtoto wako, Mungu ni mwaminifu nimeona wadada wenye watoto wawili wakiolewa ndoa tena ya Heshima, kwahiyo usishushe viwango vya Mungu, mjue kwanza Mungu na umwamini kwamba anakuwazia mema , usitengeneza Muujiza , acha mtenda miujiza akutendee na hapa hutaishi maisha ya majuto.

 

 

Haleluya asante sana kwa kuwa pamoja nasi leo,nafikiri Roho Mtakatifu ataendelea kukufundisha Zaidi hili somo na utalielewa, Kitu kikubwa nataka nikuombe usikate Tamaa Mungu wetu ni wa Majira na Nyakati, Ujue wakati wako unakuja tutakula tu Plau na kuvaa Sare haleluyaa, Tembea kwa Ushindi, Usiwe na Hofu,UTAOLEWA NA KUOA TU kama ndio desire yako, maana yeye ndio anatupa Desires of our heart, Aminaaa

 

Tuonane Tena wiki Ijayo mambo mazuri yanakuja, Haleluyaaa

 

MBARIKIWE,

 

Endelea kutembelea Rejoice and Rejoice Blog mengi na mengi sana yanakuja, Mungu anafanya mambo makubwa sana!

 

No comments:

Post a Comment