Friday, September 27, 2013

There is No Glory without Story,Hakuna Taji ya Utukufu pasipo Taji ya Mwiba by Frida Blessings James


 

UNAPITIA KIPINDI GANI KATIKA MAISHA YAKO???

TAMBUA JINSI YA KUISHINDA SAA YA MAMLAKA YA GIZA!

Hakuna mwanadamu asiyepitia kipindi hiki, usipoishinda saa hii itakushinda! Usipoiharibu itakuharibu Luka 22:52-53. Mamlaka hii ya giza inaweza kujifunua kazini, kwenye jamii/familia-nyumbani hata katika huduma au katika nchi.

Ninamaanisha nini nikisema saa ya mamlaka ya giza? Ni wakati unapopitia kipindi kigumu maishani kiasi cha kutamani kujikimbia/ kujiua au kukataa tamaa na wale uliowategemea wakakukimbia na kukaa mbali na wakati huo unaweza kuona pia Mungu amekuacha kwani atakaa kimya ili kuipima imani yako je unamwangalia yeye au tatizo.

Mamlaka hii ina majira yake na ndio maana inaitwa saa ya mamlaka ya giza.Inatumika na mtu au watu. Pia inatabia ya kukutenga na watu ili ikupate na ikumalize kwani hata uliowategemea watakaa pembeni. Ila lazima ujue hata kama wote watakimbia lazima Simon wa Kirene atokee atakuja mtu usiyemtegemea atakayeletwa na Mungu. Mfano halisi wakati ule wa Yesu , Saa ya mamlaka ya giza ilipofika kwa Yesu aliitambua. Petro alikaa pembeni akasema simfahamu mtu huyu, Yuda alimsaliti. Pia wale Mitume waliposhindwa kuomba Mungu aligusa watu, kuna wakina mama waliokuwa wakilia na kuomboleza, walimfuata Yesu na kumywesha maji.

Kumbuka saa hiyo ni saa ya kudhalilishwa, ni saa ya matusi. Kutakuwa na kusalitiwa unaweza kugeukwa na mtu uliyemtegemea sana,anaweza kuwa ndugu, mke, mume, mtoto, mzazi, rafiki,mpendwa hata mtumishi mwenzako n.k. Saa hiyo ikifika watasema unajifanya unajua kuomba na kuombea watu, watasema eti anajidai Mungu anamtumia embu fanya muujiza tuone. Watakukejeli. Watasema anajifanya ana uwezo, ni mzuri sana maneno kama hayo hayakosekani. Saa hii ilipotokea kwa Yusuph mpaka ndugu walimuuza lakini aliposimama na Mungu alifanikiwa na utukufu wa Mungu ukamfunika. Shetani alimletea majaribu mengi ili amuangushe lakini alijitambua akamshinda.Hakuna taji ya utukufu pasipo taji ya mwiba! Yusuph alipitia mateso mengi sana lakini alipoweka tumaini lake kwa Bwana alishinda.

Thursday, September 26, 2013

John Lisu kufanya Tamasha Kubwa la Kusifu na Kuabudu na DVD Live Recording ya "Uko Hapa"



Live recording ya DVD ya UKO HAPA (Albamu) ya mwimbaji maarufu wa nyimbo za Injili nchini Tanzania John Lisu inategemewa kufanyika tarehe 6 October 2013.


Tukio hilo litakuwa ni Tamasha la Sifa na Kuabudu ambalo litakuwa la tofauti kabisa na matamasha yote ya John Lisu ambayo umewahi kuhudhuria na si tamasha tu bali ni ibada ya kumwita Mungu na kila mmoja ategemee kukutana na Mungu siku hiyo.

Tamasha hilo litafanyika katika ukumbi wa Kanisa la CCC UPANGA ( Opposite Mzumbe University) .

Linategemewa kusindikizwa na waimbaji mbalimbali kama vile Christina Shusho, Neema Gospel Choir, Paul Clement, Bomby Jonson, Pastor Safari na wengine wengi.

Kiingilio cha 20,000/= VIP, 10,000/= KAWAIDA na 3,000/=WATOTO

Usipange kukosa na Mungu Akubariki

 

Monday, September 23, 2013

Non-Muslims Targeted in Deadly Kenya Mall Attack, Witnesses Say


A general view shows cars parked at the Westgate shopping mall during a shootout between armed men and the police in Nairobi September 22, 2013. Kenyan security forces were locked in a stand-off on Sunday with gunmen who killed at least 39 people at the upmarket shopping mall in the Kenyan capital, and it was still unclear how many hostages the al Qaeda-linked militants were holding. Source: REUTERS/Thomas Mukoya, Kenya
 
 

Gunmen carrying grenades and automatic weapons attacked a shopping mall in Nairobi on Saturday, leaving at least 30 people dead. Westgate Mall is an upscale shopping destination, popular with expatriates in Kenya’s capital city.

The Red Cross has reported that 30 people have died in the attack, and a Kenyan government official says that at least 100 people are injured. One suspected gunman is reportedly dead after a clash with police.

Al-Shabaab, an al-Qaeda-linked militant group based in neighboring Somalia, has claimed responsibility for the deadly attack in which gunmen targeted non-Muslims.

The militant group took responsibility for the attack on Twitter hours after gunmen entered the mall. “The Mujahideen entered #WestgateMall today at around noon and are still inside the mall,” the group posted, according to CNN.

The group’s Twitter account, followed by some 6,000 people (including many journalists) had been suspended earlier this month.

Journalist Martin Cuddihy of the Australian Broadcasting Corp was at the scene of the attacks. He reports that authorities are saying as many as 36 hostages are still being held by the gunmen inside the mall.

Thursday, September 19, 2013

Je Unataka Kufanya Biashara?


 


Je unapenda kuongea na watu, kujipatia marafiki wapya?

 

Je unapenda kuendesha biashara yako binafsi?

 

Je unataka kipato kitakachokuweka huru.

 

Tukutane Makumbusho ya Taifa, Jirani na IFM.

Tarehe : 21/09/2013

 

Muda: saa saba mchana mpaka saa kumi jioni.

 

 Siyo biashara ya mtandao

Wednesday, September 18, 2013

Uchumba hadi Ndoa: Ni Vizuri Watarajiwa kukubaliana juu ya mipaka watakayokuwa nayo kwa Ndugu wa pande zote mbili



 

Shalom Mtu wa Mungu, leo nakuletea somo muhimu sana juu ya kukubaliana na mwenzi wako jinsi mtakavyokuwa mnaishi na ndugu zenu, yaani wakwe kwa upande wa mwanaume na mwanamke pia.

Ni muhimu mkaweka  msingi mapema maana wazazi na ndugu za pande zote mbili ni muhimu sana sana kwenu wala hawahitajiki kuupuuziwa ila tu msipoweka mipaka inaweza kuleta shida kubwa sana katika maisha yenu ya huko mbele mtakapokuwa mmefunga ndoa.

Wakati mwingine ndugu za pande zote mbili wamekuwa wakijisahau na kufikiri wana nafasi ya kuamua juu ya maisha yenu kama wanandoa. Lakini katika Biblia tunaona kuna mifano mingi jinsi wanandoa walivyoishi vizuri na wakwe zao kukawa na uhusiano mzuri kati ya wakwe na mkwe kama Ruth na Naomi walivyopendwa na kuishi vizuri na wakwe zao.

Lakini pia tunaona jinsi ambavyo Mfalme Daudi alivyopata shida na baba mkwe wake Mfalme Sauli hadi Sauli akataka kumuua Daudi.


Mahusiano mabaya kati ya mkwe na wakwe yanaweza kusababisha wanandoa kuishi kwa shida kubwa sana na mara nyingine imesababisha ndoa kuvunjika kabisa na kuleta chukizo mbele za Mungu.

Sasa ili kuepusha hayo ndio maana tuko hapa leo kukuambia kwamba msije mkajisahau mkaongelea tu jinsi mtakavyojenga Masaki au Kibada bila Kuzungumzia jambo hili mapema maana kama usipoliweka sawa hutaishi kwa Raha, Ninaposema Ndugu hapa namaanisha ni mama,baba,kaka,dada,shangazi,mjomba,bibi ,babu na ndugu wengine wa kwako wewe au wa mwenzi wako pamoja na uzao wao.

Zingatieni yafuatayo ili kuepusha hiyo migogoro inayosababishwa na ndugu;

 

1. Zungumza na Mwenzako

Mzungumze jinsi mtakavyoweka mipaka kwa ndugu zenu wote itayaepusha ndugu kuingilia mahusiano yenu

Kwa mfano sikilizeni ushauri kutoka kwa wakwe maana pia ni mzuri sana kwasababu wao kwanza wameona mengi kuliko nyie ila kabla ya kufanya maamuzi make chini mkubaliane lipi mfanye au lipi mliache kwanza. Kwa kufanya hivyo mtakuwa na mahusiano mazuri maana mmeshirikishana kwenye maamuzi juu ya mashauri mliyopata.                             

Ni hatari sana ukapigiwa simu na mama au baba au mjomba wako kwamba mwanangu kuna kiwanja huku Mwabepande wewe kwa vile ulikuwa na hela Bank ukaikimbizia huko ukanunua bila kumuambia mwenzako, halafu baadae ajue kwamba umemruka katika maamuzi . Mshirikishe maana ndio unategemea kuishi naye anaweza kukupa ushauri mzuri ambao utaweza kupata kitu kizuri na cha thamani na saa nyingine kukuepusha na hasara.

Tuesday, September 17, 2013

Your Change is Coming by Pastor Dondo


Today I will speak on three things that God Uses to change a Man


Our Opening Scripture comes from Genesis 17: 1-8

17 When Abram was ninety-nine years old, the Lord appeared to him and said, “I am God Almighty[a]; walk before me faithfully and be blameless. 2 Then I will make my covenant between me and you and will greatly increase your numbers.”

3 Abram fell facedown, and God said to him, 4 “As for me, this is my covenant with you: You will be the father of many nations. 5 No longer will you be called Abram[b]; your name will be Abraham,[c] for I have made you a father of many nations. 6 I will make you very fruitful; I will make nations of you, and kings will come from you. 7 I will establish my covenant as an everlasting covenant between me and you and your descendants after you for the generations to come, to be your God and the God of your descendants after you. 8 The whole land of Canaan, where you now reside as a foreigner, I will give as an everlasting possession to you and your descendants after you; and I will be their God.”


God changes the name of Abram to Abraham

The following are steps that God used to Change Abraham;

1. He Communicated to Abraham

God is never quite he speaks to people every day through his word, Some people are waiting for Prophets to say a word of God to them and devil understanding their desire he sometimes sent False Prophets to them that is why it is very important for a Christian to read the Word of God.

Hebrew 10: 25 not giving up meeting together, as some are in the habit of doing, but encouraging one another—and all the more as you see the Day approaching

Identify yourself to a church, be responsible to your Pastor. It is very dangerous to a member of Universal Church meaning you don’t belong to any church.

Look for a local church and be a responsible member there it is very important for your Christian Growth.

Some Christians are not faithful in giving their tithes and offering

And sometimes some Christians cannot be trusted, non-believers are more faithful than us

This morning God demand a change, we should be honest to God and ourselves

Friday, September 13, 2013

Hildelly Straight Film inawaletea Uzinduzi wa Movie yao ya Kwanza


 


Hidelly Straight Film inategemea kuzindua Movie yao kwanza inayojulikana kwa Jina la He Hurts Me.

Katika mazungumzo ambayo blog imefanya na Mkurugenzi wa Hildelly Straight Film mwanamama Hilda Ngaja ambaye ameamua kujitosa katika ulimwengu wa Movie na Studio yake mwenyewe. Uzinduzi huo unategemewa kufanyika  Kesho tarehe 14/09/2013, Katika Hotel ya Mbezi Garden iliyoko eneo la Mbezi Makonde.

Uzinduzi huo utaanza kuanzia saa moja usiku hadi saa nne za Usiku.

Ticket zitapatikana mlangoni kwa gharama nafuu kama ifuatavyo:

          Single 40,000 Tsh

          Double 60,000 Tsh

          VIP 100,000 Tsh

          Meza ya watu 10 25,000 Tsh

Ukitaka kubook Meza na maelezo mengine Zaidi piga namba hizi 0784 670746

Wote Mnakaribishwa kumwezesha mwanamama huyu aliyethubutu kuingia katika tasnia hii ya Movie.

 

Wednesday, September 11, 2013

Umuhimu wa Mwamini kutambua nafasi aliyo nayo


Leo nimejifunza kitu cha Ajabu katika Lunch Hour Fellowship naona ni vizuri nikakushirikisha.

Umuhimu wa Mwamini kutambua nafasi aliyo nayo lililohubiriwa na Bishop Lubala.

Kuna tatizo kubwa sana la mwamini kutojua nafasi ambayo Mungu ametupa. Waamini tunashindwa kutumia kanuni za kuishi hapa duniani ambazo Mungu ametupa matokea yake waamini tunaishi kama watu wengine tu wasio mjua Mungu wakati sisi tunacho kitu cha tofauti na cha thamani sana.

Kitu kinachozangaza ni jinsi ambavyo mwamini anajiita Mwamini yaani mtu aliyempokea Kristo lakini anashindwa kuamini Neno la Mungu.

Kama wewe ni Mwamini na umempokea Yesu katika Maisha yako jiulize maswali yafuatayo;

1.      Mwamini ni Nani

2.      Faida za Kuwa Mwamini

3.      Vitu gani vitakusaidia uwe mwamini Mzuri

4.      Kwanini unakuwa na hofu wakati wewe ni mwamini

Tusome Neno la Mungu kutoka Waraka wa Kwanza wa Petro 2: 5-10

Monday, September 9, 2013

62% of Evangelical Pastors Oppose Syria Strike, NAE Says


The National Association of Evangelicals conducted a poll of its member pastors and found that 62.5 percent oppose U.S. military intervention in the Syrian civil war.

"Should Congress authorize direct U.S. military intervention in Syria?" the survey asked. Only 37.5 percent answered "yes," NAE President Leith Anderson announced in a statement to Jonathan Merritt at Religion News Service.

The National Association of Evangelicals represents 40 evangelical Christian denominations and over 45,000 local churches. Not all evangelical denominations are NAE members, though.

The largest evangelical denomination, the Southern Baptist Convention, for instance, is not a member. So, the views of Southern Baptist pastors would not be included in the results. (Russell Moore, president of the Southern Baptist Convention's Ethics and Religious Liberty Commission, does not support a military strike against Syria.)

Friday, September 6, 2013

Apostle Anselm Madubuko & Emmy Kosgei (Kenyan Gospel Artiste) White Wedding



VOWS.jpg

Apostle Madubuko recites his wedding vows



Award-winning Gospel songbird Emmy Kosgei on Saturday walked down the aisle in a white wedding at Windsor Golf Club after a successful traditional wedding at Kelelwa village last Thursday.

Guests were later treated to a grand reception at Nairobi’s Safari Park Hotel accompanied by performances from top Gospel artistes.
Another wedding is set to go down in Lagos in a week’s time. The couple has also fixed its wedding thanksgiving on Sunday, September 15th at Revival Assembly in Nigeria. Here are photos from the Saturday event;

CLERGY.jpg
Some of the famous clergymen and women that attended the wedding
DENA.jpg
(L-R) Becky Muikia, Kanze Dena, Nancy Kihenia and Lulu Hassan
EUNICE.jpg
Gospel worship singer Eunice Njeri
GADGETS.jpg
A section of the congregation at the colourful wedding
GROOM.jpg
Bishop. Dr Arthur Kitonga (C) officiates the wedding ceremony

Wednesday, September 4, 2013

Uchumba hadi Ndoa: Mjadili mngependa kuwa na watoto wangapi




Karibu Katika Somo letu la Uchumba hadi Ndoa, katika mtiririko wa vitu muhimu vya kuangalia unapojiandaa kuwa na mwezi wako wa maisha. Leo tutaangalia jambo ambalo ni muhimu japo watu wengine wanaweza kulisahau halafu baadae linakuja kuleta matatizo.

Mnapokuwa katika kipindi cha uchumba ni vizuri mkazungumza idadi ya watoto ambao mtapenda kuwa nao katika ndoa yenu, najua mtu anaweza kusema kama je hatutapata watoto? Au unampangia Mungu? Haya ni maswala ya Imani lazima twende kwa Imani hivyohivyo maana kwanza sio wachumba wote lazima waje waoane kwa hiyo kama mnavyokuwa katika Imani kwamba mtafunga ndoa ndivyo hivyohivyo mnatakiwa kumwamini Mungu kwamba atawabariki na watoto.

Kubalianeni idadi maana isije ikawa mwingine labda hataki mtoto kabisa na mwenzi wake anataka watoto watano sasa hapo unafikiri wakifunga ndoa itakuwaje huko ndani. Nilishapata ushuhuda kuna mkaka alikuwa anataka watoto wanne lakini mwenzi wake alikuwa anataka aolewe na mtu ambaye wataishi bila kuwa na mtoto. Kwasababu walijadili kabla ya ndoa na kila mtu akajua mahitaji ya mwenzake kwenye jambo hilo, ilibidi wazungumze na kushauriana na mwisho wakakubaliana namba fulani. Hebu fikiria wasingejadili ingekuwaje mtu wa Mungu.

Mungu akusaidie uweze kufanya maamuzi sahihi maana kwakweli bora tu uchumba uvunjike lakini sio ndoa maana ndoa zetu sisi tunajua ni za milele ni Kifo tu kinazitenganisha.

 

Endelea Kutembelea Rejoice and Rejoice, Mambo mazuri yanakuja yatakuinua, kukubariki na kubadilisha kabisa maisha yako najua kuna mahali tunaelekea, Amen


Tuesday, September 3, 2013

Emmanuel Akyoo and Gloria Wedding

 
Congratulation Mr and Mrs Emanuel Akyoo

 
At Usa River Lutheran Church
 
 

The Parents, Bishop Akyoo & Mama and Mr & Mrs Shali 




 
 
I like the green environment it is Wow, Arusha my home....



Nice

Monday, September 2, 2013

Tweka Kilindini na Fred Raphael


 

Neno la kutuongoza linatoka katika Luka 5: 1-8 “1 Siku moja Yesu alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti, na watu wengi walikuwa wamemzunguka wakisongana wanalisikiliza neno la Mungu.

 2 Akaona mashua mbili ukingoni mwa ziwa; wavuvi wenyewe walikuwa wametoka, wanaosha nyavu zao.

3 Baada ya Yesu kuingia katika mashua moja, iliyokuwa ya Simoni, alimtaka Simoni aisogeze majini, mbali kidogo na ukingo wa ziwa. Akaketi, akafundisha umati wa watu akiwa ndani ya mashua.

4 Alipomaliza kufundisha, akamwambia Simoni, "Peleka mashua mpaka kilindini, mkatupe nyavu zenu mpate kuvua samaki."

5 Simoni akamjibu, "Bwana, tumejitahidi kuvua samaki usiku kucha bila kupata kitu, lakini kwa kuwa umesema, nitatupa nyavu."

 6 Baada ya kufanya hivyo, wakavua samaki wengi, hata nyavu zao zikaanza kukatika.

7 Wakawaita wenzao waliokuwa katika mashua nyingine waje kuwasaidia. Wakaja, wakazijaza mashua zote mbili samaki, hata karibu zingezama. 8 Simoni Petro alipoona hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu akisema, "Ondoka mbele yangu, ee Bwana, kwa kuwa mimi ni mwenye dhambi!”

Vitu vizuri haviko juu juu viko kilindini yaani chini kabisa.

Samaki wazuri wako kilindini,madini ya thamani sana halikadhalika yanapatikana kwa kuchimba chini sana.

Kutoka neno tulilosoma hapo juu inaonekana hao watu walikuwa wametumia akili zao sana lakini hawakufanikiwa.

Kuna mahali uzoefu, elimu, na mtandao (connection) ulizonazo zinagota hapo sasa ndio Mungu anachukua nafasi yake.

Mambo mazuri ya Mungu hayako juu juu tu pia inabidi kutweka kilindini.

Kama utampa Bwana nafasi katika maisha yako kwa mshahara uleule, kazi , elimu ulivyonavyo sasa unaweza kufanya makubwa kwasababu umevikabidhi kwake.

Mruhusu Yesu atakufunulia, atakupitisha, utaona vitu ambavyo hujawahi kupata.

Ukitazama katika neno la Mungu utaona uhalisia wako wewe ni nani, Akaacha vitu akamfuata yeye anayeweza kukupa vitu.

Inawezekana umejaribu mengi kwa uwezo wako lakini kwa Neno la Bwana inawezekana.