Thursday, May 16, 2013

Vitu muhimu vya kuangalia unapojiandaa kuwa au kutafuta mwenzi wa Maisha-Part IV



 
Haya wapendwa wangu,poleni kwanza maana wiki ijayo sikutokea nilikuwa busy kidogo na huduma,yote ni katika kuujenga mwili wa Kristo

Leo tunaendelea na vitu muhimu  vya kuangalia kwa mtu anayetarajia kuwa mwenzi wako. Tulianza na jambo muhimu juu ya Uhusiano wake na Mungu tukachambua vipengele mbalimbali katika hapo inawezekana kabisa sijamaliza vyotee maana eneo la uhusiano wa mtu na Mungu ni pana sana,ila kwa kifupi yale ni mambo muhimu ya kuzingatia.

Tuendelee...


1.      Historia yake ya nyuma ikoje

Huyu mwenza ni vizuri ukajua historia yake ya nyuma kama utakuwa na neema akuambie yeye mwenyewe au ujiweke kuwa mchunguzi wa kujitegemea katika hilo maana si ni jambo la maisha yako,kwahiyo lazima uhakikishe linakupa amani.

Nimeona vilio katika ndoa watu wanakuja kujua kwamba wenzi wao walikuwa hivi na vile wakati tayari wameshaingia,mtu anaona kama vile mwenzake amemchezea picha yaani filamu kabisa,kwasababu niambie mwenzangu umeshaingia ndio unajua hee mpendwa huyu kumbe ana watoto,au alikuwaga mwizi,jambazi,mahusiano e.t.c. Kwakweli inauma sana kujua jambo hilo kwa kuchelewa au ukiwa tayari kwenye ndoa.

Ni vizuri mtu ujue mapema halafu ujievaluate kama unaweza kuyabeba mambo hayo,ujipime mapema kabisa hivi kweli mimi jamani nitaweza kuolewa au kumuoa mtu mwenye historia ya namna hii,je nitaweza kulelea mtoto wa mtu mwingine? Je nitaweza kuibeba aibu hii ya mwenzi wangu au nitajisikia hata vibaya kutembea nae maana yeye alikuwa na historia hii.

 

Ukiona huwezi usijitese na pia sio vizuri uingie na ukaanze kumtesa mwenzako na maneno ya manyanyaso ooh ndio maana ulikuwa a,b,c...z, mpendwa kuwa muwazi mapema

Ili kuwa na amani na kutoingia katika mahusiano halafu yavunjike kwa ajili ya mambo ya historia zingatia haya;

 

a.      Uliza historia mapema

Ni vizuri katika hatua ya mwanzo kabisa ya urafiki kabla hamjafika kutambulishana kwa wazazi,ndugu na jamaa kujua kwa uwazi kabisa historia ya huyo anayetaka kuwa mwenzi wako. Hii itakusaidia kuamua kuendelea au kuachana na mahusiano hayo mapema. Itakupunguzia kama sio kukuepushia kabisa na machungu ambayo yangejitokeza huko mbeleni

b.      Kupata muda wa kutosha kuijua na kutathimini hiyo historia
Jipe muda usikimbie sana,usifanya fasta fasta,utakua mtu anakuja kwa spidi kali sana anataka aoe kumbe kuna kitu ameficha kikubwa anataka fasta usipate hata muda wa kukihisi hicho kitu kuwa makini mpendwa.

Na ujue kabisa kwa akili zako hutaweza ila Mungu atakuwezesha,na atakuwezesha tu utakapokuwa na mahusiano mazuri na yeye,Amen! Hebu tusome pamoja huu msitari kutoka katika Yeremia 33:3 “ Niite nami nitakuitikia nami nitakuonyesha mambo makubwa usiyoyajua” ukiangalia huu mstari utaona jinsi Mungu anavyosema kwamba muite na yeye atakuitikia na kisha atakuonyesha mambo makubwa usiyoyajua. Kwa hiyo hata kama kuna vitu anaficha hataki uvijue ukimwita Yesu atakuonyesha mpendwa wala usiwe na wasiwasi. Mungu ni mwaminifu sana sana yaani ninayo kila sababu ya kusema hivyo maana nimeuona uaminifu wake katika mambo mbalimbali kwangu na watu wengine walioamua kumtegemea.

Mungu anaweza mpendwa mtegemee tu yeye peke yake na uweza wake.
 

2.      Angalia jinsi anavyoishi na watu

Ukitaka kujua tabia halisi ya mtu angalia jinsi anavyoishi au kutenda kwa watu ambao hawajui au watu wa hali ya chini. Kama mmekwenda mahali kunywa juice angalia jinsi anavyomwambia au kumkosoa yule muhudumu kama amesahau kitu, je anamuambia kwa kumwelimisha kwamba amekosea? Au anamwambia kwa dharau na kumkashifu? Hapo utajua kabisa huyu mtu mmh nikija kukosa nitakoma.

Je kama ni mtu ambaye ana uwezo wa kifedha au amesoma kiasi ,akikutana na watu ambao hawana uwezo au ambao hawajasoma kama yeye anaongeaje nao,anawajali,anawaelimisha? au ndio anawaonyesha dharau kubwa kwasababu yuko katika kiwango cha tofauti na wao.

Neno la Mungu katika Mithali 17: 5 linasema Amdhihakiye maskini humsuta Muumba wake; Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu”.

Mtu anayemdharau masikini au mtu mwenye shida ni chukizo mbele za Mungu na ataadhibiwa. Kuwa makini na mtu wa jinsi hii maana atakuja kukuletea matatizo baadae. Ila pamoja na yote hata kama ana hiyo tabia unaweza pia kumshauri kama ni mtu ambaye anapenda kubadilika ataiacha ila kama ni mtu anayejihesabia haki hataiacha hapo ndio inabidi uchukue hatua uamue kama unaendelea na huo uhusiano au lah.

 

 
Tutaendelea wiki ijayo na vitu muhimu vya kuangalia kwa mtu unayetegemea awe mwezi wako.

 
Karibu tena na Mungu akusaidia unapoinza hii safari uimalize kama yeye alivyokusudia,Amen

 

 

No comments:

Post a Comment