Tuesday, September 4, 2012

Philippians 4:4 "Rejoice in the Lord always. I will say it again: Rejoice"!


Wapendwa kama mstari unavyosema hapo juu,kwakweli Rejoice in the Lord! Haijalishi ni Jaribu gani unapitia please Rejoice because you have Christ in you na kama neno la Mungu linavyosema katika Colossians 1:27 “Christ in you the Hope of Glory,hata kama umekaa miaka mingi bila kupata mtoto na wakwe zakwe na watu wengine wanakusema vibaya wanakucheka simama na jipige kifua na ujiambie huu mstari Christ in me the hope of Glory. Yawezekana umekwenda hospital wakakuambia una ugonjwa ambao hautibiki usijali jipe Moyo na ujue kwamba Madaktari wa duniani wana elimu ya duniani tu ya sayansi na wao sio final..yuko Bwana Yesu anayejua mustakabali wako atakushindia nayeye katika maneno yake amesema kwamba kwa kupigwa kwake Bwana Yesu sisi tuliponywa,unachotakiwa wewe ndugu yangu ni kuamini tu,au wazungu wanasema have Faith,Imani inaweza kufanya yale mambo yanayoonekana kwamba ni magumu kuwa mepesi kwako. Maneno ya Mungu yanasema kwa Imani Sarah alipata mimba akiwa ameshapita kile kipindi ambacho kina mama hawawezi tena ku-concieve akiwa na umri wa miaka 90 hebu fikiria mpendwa wangu kweli hilo jaribu lako laweza kuzidi hili kweli jamani….inuka na songa mbele….

Je una madeni?Au unahitaji mwenza wa maisha? Je mke au mume wako amekimbia au amebadilika? Yeye alikufa msalabani na akasema imekwisha,mwamini Yesu yeye ni mwaminifu atabadilisha historia ya maisha yak oleo mpendwa wangu…..SONGA MBELE…Naupenda sana ume wimbo wa ‘Hakuna jaribu kumbwa hawezi ondoooa… sikumbuki vizuri nani ameimba but unatia moyo sana….

Kitu cha ajabu sana kuhusu NENO LA MUNGU ni hai,ukitamka linakwenda kubadilisha situation…..tutakavyokuwa tunaendelea nitashare shuhuda mbalimbali uone jinsi Mungu alivyo mkuu na mwaminifu katika ahadi zake….


 

Hallelujah karibu ~ Rejoice and Rejoice…..

No comments:

Post a Comment